• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Singida District Council
Singida District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na LIshe
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI
    • Vitengo
      • TEHAMA na TAKWIMU
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • Michezo , Utamaduni na Sanaa
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, uongozi na mipango
      • Uchumi, ujenzi na mazingira
      • Huduma za jamii
      • VVU UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya madiwani
      • Kumuona mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

MAMA SAMIA LEGAL AID CAMPAIGN YAZINDULIWA RASMI SINGIDA

Posted on: January 10th, 2024

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe Pindi Hazara Chana leo tarehe 10/01/2024 amezindua rasmi kampeni ya kitaifa ya msaada wa kisheria - Mama Samia Legal Aid Campaign katika Mkoa wa Singida kwa lengo la kuwafikia Wananchi wasio na uwezo wa kupata huduma hizo.


Mkoa wa Singida unakuwa ni Mkoa wa sita kuzindua huduma hizi ukiwa umetanguliwa na Mkoa wa Dodoma,Manyara,Shinyanga,Ruvuma na Simiyu ambapo huduma za msaada wa kisheria zitatolewa katika Kata na Mitaa yote ya Mkoa huu.


Mhe. Pindi Chana ameelezea nia ya Mhe. Rais kutaka kuhakikisha kwamba kila Mwananchi anakuwa na ufahamu wa masuala ya Sheria ikiwemo Haki na Wajibu wake na kwamba kila Mwananchi anaifikia haki na kwa wale wasiokuwa na uwezo wa kumudu Gharama za Watoa huduma za Kisheria(Mawakili) basi waweze kufikia kupitia huduma hizi za msaada wa Kisheria.


Mheshimiwa Rais aliunda Bodi ya kusimamia shughuli za msaada wa kisheria ambapo Huduma  hizi zinaratibiwa na Serikali kupitia Wizara ya Katiba na Sheria, Utaratibu unaosimamiwa vizuri na uko katika ngazi zote za Mikoa na Wilaya ili kuhakikisha upatikanaji wa Huduma za msaada wa kisheria kwa wakati hata kule pembezoni kabisa mwa nchi.


Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Waziri wa Sheria na Katiba Mkuu wa Mkoa wa Singida Mhe Peter Serukamba alimuhakikishia kwamba Mkoa wa Singida unaendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan katika nia yake thabiti ya kuondoka kadhia na viashiria vyote vya ukatili wa kijinsia na ulinzi wa haki za binadamu katika jamii pamoja na kushughulikia kero za wananchi wa Tanzania.


"Uzinduzi wa kampeni hii ni uthibitisho tosha kuwa Mhe Rais ni Muumini wa kweli na haki ,na haki siku zote huliinua Taifa, Mhe Rais ameamua kuliinua Taifa letu juu na Taifa lolote linaloamini katika haki ni Taifa lenye Maendeleo"

Matangazo

  • TANGAZO LA KUKODISHWA KWA SHAMBA LA MBEGU LA MPAMBAA September 16, 2025
  • TANGAZO LA WATUMISHI KUHUSU WCF September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI August 30, 2025
  • TANGAZO LA FURSA ZA KUTOA HUDUMA ZA CHAKULA (CATERING) KATIKA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA September 01, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKUTANO MAALUM WA MAANDALIZI YA MSIMU WA KILIMO, WILAYA YA SINGIDA.

    October 03, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, YAFANYA UKAGUZI.

    October 02, 2025
  • MHE. GONDWE ATEMBELEA MIRADI YA LISHE KATIKA SHULE 3 ZA SEKONDARI.

    September 29, 2025
  • USAFI WA MAZINGIRA WAFANYIKA, KATA YA MUGHAMO

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video

WATUMISHI WAPYA WAASWA KUWEKA AKIBA
More Videos

Kurasa za karibu

  • Matangazo
  • Habari
  • Matukio

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti kuu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - Utumishi
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa - Singida
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Jengo la Utawala Kijiji cha Mwahango Kata ya Ilongero

    Anuani ya Posta: Box 27, Singida

    Simu: +25526502252

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded.singidadc@singida.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Singida. Haki zote zimehifadhiwa.