• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Singida District Council
Singida District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na LIshe
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI
    • Vitengo
      • TEHAMA na TAKWIMU
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • Michezo , Utamaduni na Sanaa
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, uongozi na mipango
      • Uchumi, ujenzi na mazingira
      • Huduma za jamii
      • VVU UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya madiwani
      • Kumuona mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

KATIBU TAWALA MKOA WA SINGIDA ATOA VYETI VYA PONGEZI KWA WATENDAJI WALIOFANYA VIZURI

Posted on: August 11th, 2023

Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt Fatuma Mganga ametoa Vyeti vya Pongezi kwa Ukusanyaji bora wa Mapato ya Halmashauri kwa Watendaji wa Kata saba waliofanya vizuri zaidi, Watendaji wa Kata waliozawadiwa ni Faraja Manase wa kata ya Mudida, Moses Daniel wa kata ya  Makuro,Fransic Hoyo wa kata ya Mtinko, Hussein Athumani  wa kata ya Mwasauya,Narcis Weruma wa kata ya Ughandi,Elizabeth Mangu wa kata ya Ntonge na Juma Saadi wa kata ya Mughunga. Hafla hiyo fupi imefanyika wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kwa robo ya nne 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa Shule ya sekondari Ilongero.

Akitoa Salamu za Mkoa kwenye Baraza  Dkt Fatuma Mganga amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Ndg Ester Anania Chaula kwa Ubora na Umahiri katika utekelezaji wa miradi ya BOOST pia amelipongeza Baraza la Madiwani kwa maamuzi sahihi ya kuhamia kwenye Jengo jipya la Utawala lilipo katika kijiji cha Mwahango kata ya Ilongero na kuliomba Baraza hilo kuorodhesha miradi yote ambayo ilipata fedha na haikuweza kukamilika ili vikao vya kamati ya Fedha ,Uongozi na Mipango ipange mikakati ya ukamilishwaji wake.Akiongelea  Miradi ya Serikali inayoendelea kutekelezwa Dkt Mganga amesisitiza kuzingatia zaidi ubora wa miradi hiyo kwa kutumia mafundi wenye uweledi mkubwa na sio tu bora fundi anayetokea kwenye jamii yetu, '' Miradi ya Serikali sio miradi ya kujifunzia '' alisisitiza.

Pia Katibu Tawala wa Mkoa amewakumbusha Madiwani kupitia Kamati ya Elimu, Afya na Maji kuangalia njia bora za kuongeza ufaulu kwa wanafunzi kwenye wilaya yetu kwani kuna viashiria vya kushuka kwa kiwango cha elimu hasa katika mazoezi ya upimaji(Mock). Akilinganisha na kiwango cha ufaulu kwa miaka ya nyuma Dkt Mganga amesema zamani ufaulu ulikuwa asilimia 96 lakini kwa sasa ufaulu umeshuka hadi asilimia 60 na baadhi ya maeneo uko kwenye asilimia 30. Ameliomba baraza la Madiwani limuunge mkono kwenye vita vya kuongeza ufaulu kwa mkoa wa Singida nikimnukuu Dkt Mganga amesema " Hili swala la Elimu ni changamoto kwa hakika majbu ya kumjibu Mheshimiwa Rais kwamba tunasema asante kwa Miradi hii, Majibu yake nikutoa watoto waweze kufaulu tuwavushe waweze kuendelea katika ngazi nyingine"

Akilifunga Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida Mhe. Elia Digha amemshukuru Katibu Tawala wa Mkoa na kumuahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyowasilishwa.


Matangazo

  • TANGAZO LA BVR May 11, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI YA KAZI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA April 17, 2025
  • MAENEO YA UWEKEZAJI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA January 03, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA KAZI ZA MUDA July 17, 2022
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAKUU WA IDARA NA VITENGO WA HALMASHAURI YA SINGIDA WAPATA MAFUNZO KUHUSU USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI KATIKA UWEKEZAJI

    April 03, 2025
  • TAWA YATOA ELIMU YA MBINU ZA KUKABILIANA NA WANYAMA PORI

    April 03, 2025
  • HALMASHAURI YA MANISPAA KIGOMA UJIJI WATEMBELEA HALMASHAURI YA SINGIDA

    March 28, 2025
  • MKUU WA WILAYA YA SINGIDA AWAASA WALIMU KUEPUKA MIKOPO UMINZA

    March 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Mgogoro wa Ardhi Tarafa ya Mgori wamaliizika
More Videos

Kurasa za karibu

  • Matangazo
  • Habari
  • Matukio

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti kuu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - Utumishi
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa - Singida
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Jengo la Utawala Kijiji cha Mwahango Kata ya Ilongero

    Anuani ya Posta: Box 27, Singida

    Simu: +25526502252

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded.singidadc@singida.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Singida. Haki zote zimehifadhiwa.