• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Singida District Council
Singida District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na LIshe
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI
    • Vitengo
      • TEHAMA na TAKWIMU
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • Michezo , Utamaduni na Sanaa
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, uongozi na mipango
      • Uchumi, ujenzi na mazingira
      • Huduma za jamii
      • VVU UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya madiwani
      • Kumuona mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

KIKAO CHA BARAZA MAALUM LA MADIWANI LA KUPITIA MPANGO WA BAJETI YA HALMASHAURI KWA MWAKA 2025/2026

Posted on: January 28th, 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida,Mhe.Elia Digha ameongoza Kikao cha Baraza maalum la Madiwani la kupitia Mpango wa Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka 2025/2026.

Kikao hicho kilichoketi leo tarehe 28/1/2025 katika ukumbi mkubwa wa mikutano uliopo katika Ofisi za Halmashauri,kimehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa serikali na Kisiasa wakiwemo, Muwakilishi wa Katibu Tawala za Mikoa,Katibu Tawala wa Wilaya ambaye alimuwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Singida,Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Maafisa Tarafa, Madiwani pamoja na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida.

Akifungua Kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri amewasisitiza Wataalamu wa Halmashauri,suala la ukusunyaji wa mapato,hususan katika zao la vitunguu ambalo linategemewa kwa kiasi kikubwa kuleta mapato makubwa.

“ Kuwa na 55% kwa kwetu kwa kipindi hiki ni kama tumejitahidi,lakini niwaombe sana Wataalamu tusilegee kwasababu tunakuja sisi asilimia kubwa ya ukusunyaji wetu unategemea mazao ya biashara,na mazao hayo ni zao la vitunguu,na kama tunavyojua bila kufika mahali salama kwenye ukusunyaji wa mapato kwenye zao la vitunguu hatutafika salama” Alisema Mhe.Digha.


Akitoa salamu kwa niaba ya  Katibu Tawala za Mikoa, Bw. Romwald Mwendi, ambaye pia ni Afisa Mipango wa Mkoa wa Singida ameishauri Halmashauri,kuhusiana na maeneo kadhaa ya kukazia katika kuboresha ukusunyaji wa mapato,ambapo moja wapo ni kutenga na kurejesha mapato yatokanayo na kilimo,mifugo na uvuvi.

“ Maeneo machache pia ambayo nataka tuendelee kuyakazia ni pamoja na kutenga na kurejesha mapato yatokanayo na kilimo, mifugo na uvuvi,ambayo tunapata vyanzo vya mapato yetu ya ndani katika Halmashauri yetu. Hivyo, 20% inayopatikana kwenye vyanzo vya kilimo irudi kuendeleza yale maeneo ya kilimo, 15% kwenye mifugo na 5% irudi kwenye uvuvi kama tuna maeneo ya uvuvi” Alisema Bw. Romwald Mwendi.

Hatahivyo, pamoja na masuala ya Bajeti na Mapato kujadiliwa, waheshimiwa Madiwani na Wataalamu wamekumbushwa masuala mbalimbali yakiwemo kuendelea kusimamia uandikishwaji wa watoto wa Shule za awali na msingi na kuwasimamia wakulima ili wapate pembejeo za kilimo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUKODISHWA KWA SHAMBA LA MBEGU LA MPAMBAA September 16, 2025
  • TANGAZO LA WATUMISHI KUHUSU WCF September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI August 30, 2025
  • TANGAZO LA FURSA ZA KUTOA HUDUMA ZA CHAKULA (CATERING) KATIKA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA September 01, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKUTANO MAALUM WA MAANDALIZI YA MSIMU WA KILIMO, WILAYA YA SINGIDA.

    October 03, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, YAFANYA UKAGUZI.

    October 02, 2025
  • MHE. GONDWE ATEMBELEA MIRADI YA LISHE KATIKA SHULE 3 ZA SEKONDARI.

    September 29, 2025
  • USAFI WA MAZINGIRA WAFANYIKA, KATA YA MUGHAMO

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video

WATUMISHI WAPYA WAASWA KUWEKA AKIBA
More Videos

Kurasa za karibu

  • Matangazo
  • Habari
  • Matukio

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti kuu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - Utumishi
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa - Singida
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Jengo la Utawala Kijiji cha Mwahango Kata ya Ilongero

    Anuani ya Posta: Box 27, Singida

    Simu: +25526502252

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded.singidadc@singida.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Singida. Haki zote zimehifadhiwa.