• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
Singida District Council
Singida District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Singida

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Idara
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu
      • Fedha na Uhasibu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
      • Huduma za Afya,Ustawi wa Jamii na LIshe
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Ujenzi na Zimamoto
      • USIMAMIZI WA TAKA NA USAFI
    • Vitengo
      • TEHAMA na TAKWIMU
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Usimamizi na Ununuzi
      • Michezo , Utamaduni na Sanaa
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, uongozi na mipango
      • Uchumi, ujenzi na mazingira
      • Huduma za jamii
      • VVU UKIMWI
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya madiwani
      • Kumuona mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa mteja
    • Mpango mkakati
    • Ripoti mbalimbali
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

KIKAO CHA WAGANGA WAFAWIDHI WA ZAHANATI NA VITUO VYA AFYA.

Posted on: April 11th, 2025

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Singida, Dk. Dorisila John, ameongoza kikao cha Waganga Wafawidhi wa vituo vya afya na zahanati zote za Halmashauri ya Wilaya ya Singida, leo tarehe 11/04/2025 katika ukumbi wa mikutano uliopo katika Hospitali ya Wilaya.


Lengo  la kikao hicho ni kujadiliana kwa pamoja masuala mbalimbali yanayohusu utoaji wa huduma za afya kwa wananchi, lakini kubwa ni kufanya tathmini kuhusu uwekezaji wa serikali katika sekta ya afya ukilinganisha na utolewaji wa huduma unavyotekelezwa na watumishi wa afya.


Pamoja na majadiliano, Dk. Dorisila amewasisitizia waganga wafawidhi, kuzingatia ubora wa utoaji wa huduma ili kuepuka kuichonganisha serikali kwa wananchi wake, hususan Mhe. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ambaye ndio kiongozi Mkuu wa Serikali.


“ Watumishi msiwe chanzo cha uchonganishi baina ya serikali na wananchi wake, kwasababu serikali imeshafanya jukumu lake, kwa zaidi ya  asilimia miamoja. Ukiangalia miundombinu imeboreshwa, vifaa tiba vipo vya kutosha, dawa zipo za kutosha, watumishi wanaongezwa kila wakati, mafunzo yanafanyika mara kwa mara, wizara inaleta Wataalamu wanaotoa mafunzo kwa watumishi ili kuwaongezea ujuzi, kwa hivyo hakuna sababu yoyote ya wananchi kutokupata huduma bora.” Alisema Dk. Dorisila.


Vilevile ametoa rai kwa waganga wafawidhi kuzingatia matumizi ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kwani hiyo ndio Muongozo wa kuwawezesha kufanya majukumu yao kwa ufanisi kulingana na kile serikali ilichoazimia kutekeleza kwa wananchi kwa upande wa sekta ya afya. Pia amewasihi kuzingatia maelekezo yanayotolewa na Viongozi, kama vile Mkuu wa Wilaya, Mwenyekiti na  Mkurugenzi wa Halmashauri ambao mara zote wamekuwa wakisisitiza utolewaji bora wa huduma za afya kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUKODISHWA KWA SHAMBA LA MBEGU LA MPAMBAA September 16, 2025
  • TANGAZO LA WATUMISHI KUHUSU WCF September 10, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI August 30, 2025
  • TANGAZO LA FURSA ZA KUTOA HUDUMA ZA CHAKULA (CATERING) KATIKA MRADI WA BOMBA LA MAFUTA September 01, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MKUTANO MAALUM WA MAANDALIZI YA MSIMU WA KILIMO, WILAYA YA SINGIDA.

    October 03, 2025
  • TIMU YA UKAGUZI KUTOKA KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOAJI, YAFANYA UKAGUZI.

    October 02, 2025
  • MHE. GONDWE ATEMBELEA MIRADI YA LISHE KATIKA SHULE 3 ZA SEKONDARI.

    September 29, 2025
  • USAFI WA MAZINGIRA WAFANYIKA, KATA YA MUGHAMO

    September 26, 2025
  • Angalia zote

Video

WATUMISHI WAPYA WAASWA KUWEKA AKIBA
More Videos

Kurasa za karibu

  • Matangazo
  • Habari
  • Matukio

Tovuti mashuhuri

  • Tovuti kuu ya Taifa
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Ofisi ya Rais - Utumishi
  • Ofisi ya Mkuu wa Mkoa - Singida
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana nasi

    Jengo la Utawala Kijiji cha Mwahango Kata ya Ilongero

    Anuani ya Posta: Box 27, Singida

    Simu: +25526502252

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded.singidadc@singida.go.tz

Mawasiliano zaidi

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Halmashauri ya Wilaya ya Singida. Haki zote zimehifadhiwa.